Moyo wangu sio mpira, mateke kuupigapiga
Usinipakulie zako hasira, mie sio yako tiba wala kinga
Ilikushinda subira, ombi langu ukalipingapinga
Kwa nilivokutumainia, ukaonelea bora kutangatanga
Moyo wangu sio danganyadanganya, umechoka kuhanywahanywa
Huba langu aminifu, na wengine Sitaki kuchanganywachanganywa
Moyo wangu hupenda kikamilifu, hata ukinyanyaswanyanyaswa
Moyo wangu mzinga wa asali kuugundua, kuila nyuki watakusumbua
Moyo wangu ni harusi, moyo wangu ni matanga
Nkikuzawadi ni kama harusi, sipoutunza ni yako majanga
Moyo wangu una wake weusi, moyo wangu una wake mwanga
Moyo wangu thamani, katu siupeani kihubahuba tena asilaniā¦

Leave a comment