Tag: Mawazo

  • Habibi

    Nimependa banati mtulivu
    Ila majibu yake naona wivu
    Nimempenda kwa moyo wangu wote
    Nikitakacho kwake ni tuwe sote
    Kaajaliwa na urembo timilifu
    Kiwa nami ntajihisi mkamilifu
    Kimwana tano kwa tano
    Kila akipita napata homa ya manjano
    Ana asili ya waja wa Mlima Kenya
    Nimwonapo nahisi kana kwamba moyo kaumenya
    Ila kumwambia nasitasita
    Nikihofia nafsi kupigwa vita
    Nifanyeje na moyo wamuita???

Design a site like this with WordPress.com
Get started